Katibu Mkuu António Guterres kupitia ukurasa wake wa Twitter amekaribisha hatua ya mfalme wa Saudi Arabia Salman bin Abdulaziz Al Saud kutoa agizo la kuondoa zuio hilo akisema ni hatua muhimu kwenye mwelekeo wa haki.
Idhaa ya Umoja wa Mataifa ilizungumza na Mohammad Naciri ambaye ni Mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na wanawake UN Women katika nchi za kiarabu ili kupata maoni yake kuhusu hatua hiyo..
"Tunaona kama hatua ya kiashiria kutoka kwa ufalme wa Saudi Arabia kuelekea kwenye fursa zaidi ya haki kwa wanawake wa Saudia kwenye ufalme huu."
Amesema kwa wanawake nchini Saudi Arabia uamuzi huo ni mwendelezo wa hatua muhimu ambazo zimekuwa zikichukuliwa na ufalme wa nchi hiyo.
"Kwa kuteua wanawake wa Saudi katika bunge la Saudia au baraza la Shura na pia kupitisha sheria kuhusu ukatili wa kingono na hatua hii ya lengo inafungua milango zaidi kuelekea usawa kwa masuala ya wanawake."
Wednesday, 27 September 2017
Umoja wa Mataifa wapongeza Saudi Arabia kwa kuruhusu wanawake kuwa madereva
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Smart Ago ni jina la blog yangu ambapo blog hii nimeianzisha kwa sababu nyingi na tofautitofauti.Ambapo miongoni mwa malengo yangu ni kuwaandalia na kuwafikishia habari mbalimbali za ndani na nje ya nchi,michezo,siasa na kutoa elimu nyingine nyingi katika jamii yangu inayonizunguka ili kuweza kuwa urahisi wa wao kutohangaika kutafuta semina pengine wengine wako vijijini ata kuangalia runinga kwao ni ngumu hivyo watapata habari kwa kuandika smartago.blogspot.com popote walipo kwa kutumia simu zao za smartphone, karibuni sana na mualike na mwenzako.
No comments:
Post a Comment