
Akizungumza kwenye uzinduzi wa mkutano wa 33 wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es salaam, amesema kwamba Madiwani hao walifahamu masharti ya kugombea nafasi hiyo, hivyo kama wameshindwa kuyatimiza ni vyema wakajiuzulu.
“Ndio maana diwani masharti tunapojaza fomu tunaambiwa lazima uwe na kazi maalum inayokupa kipato, sasa kama wapo madiwani waliojaza hiyo nafasi na hawana kazi ya kuwapa kipato, wajiuzulu udiwani”, amesema Rais Magufuli.
Leo katika hotuba iliyowasilishwa kwa Rais Magufuli ikisomwa na Mwenyekiti wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) Bwana Gulam Mkadam, waliomba kuongezewa posho za madiwani, kutoka Tsh. 300,000 hadi Tsh. 800,000 jambo ambalo Rais amelipinga.
No comments:
Post a Comment