Watu wengi wamekuwa hawafahamu wafanyaje ili kutunza betri la simu ambayo ni jipya ili lisiwahi kuaribika. Kama wewe ni miongoni mwa watu hao nakusihi uweze kuambatana nami kwani nitakueleza namna ya kuchaji betri likiwa jipya ili lisiharibike mapema.
Mara tu baada ya kununu simu. Iwashe simu hiyo kisha angalia ina asilimia ngapi ya chaji. Baada ya kuona ina asilimia ngapi, unashauriwa kufanya yafutayo;
Kama ina asilimia hamsini (50%) au zaidi usiweke simu kwenye chaji bali unatakiwa kuitumia, mpaka chaji hiyo itakofika asilimia kumi (10%) ndipo uiweke kwenye chaji.
Mara baada ya kuweka kwenye chaji hakikisha unaichaji simu hiyo kwa muda wa masaa matatu ndipo uanze kuitumia tena. Kwani baada ya masaa matatu itakuwa imejaa vizuri kwa ajili ya matumizi.
Lakini endapo umenunua simu mpya au betri jipya mara tu baada ya kuwasha ukakuta ina chaji ambayo ina asilimia arobaini na tisa (49%) kushukua chini (49%-0%) tafadhari sana usiitumie simu au betri hilo, bali iweke chaji kwa muda wa masaa matatu ndipo uanze kuitumia simu hiyo.
Lakini jambo la muhimu na lakuzingatia ni kwamba kumbuka kuichaji simu yako kila wakati kila inafika chaji kwa kiwango cha asilimia kumi (10%)
Kufanya hivi kutakusaidia sana kuweza kulitunza betri lisiwahi kuaribika mapema.
Asante sana kwa kutembelea Smart ago Blog.
Wednesday, 27 September 2017
Mbinu bora ya kuchaji betri la simu ambalo ni jipya ili lisiharibike mapema
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Smart Ago ni jina la blog yangu ambapo blog hii nimeianzisha kwa sababu nyingi na tofautitofauti.Ambapo miongoni mwa malengo yangu ni kuwaandalia na kuwafikishia habari mbalimbali za ndani na nje ya nchi,michezo,siasa na kutoa elimu nyingine nyingi katika jamii yangu inayonizunguka ili kuweza kuwa urahisi wa wao kutohangaika kutafuta semina pengine wengine wako vijijini ata kuangalia runinga kwao ni ngumu hivyo watapata habari kwa kuandika smartago.blogspot.com popote walipo kwa kutumia simu zao za smartphone, karibuni sana na mualike na mwenzako.
nice
ReplyDelete