Mwendesha mashtaka mkuu nchini Kenya, Keriako Tobiko, ameamuru uchunguzi ufanywe dhidi ya tume ya kusimamia uchaguzi nchini Kenya IEBC.
Hii ni kuhusiana na makosa yaliyofanyika wakati ilipokuwa ikishughulikia uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi uliopita.
Bwana Keriako Tobiko ameiomba idara ya polisi pamoja na tume ya kupambana na ufisadi nchini humo, kuwasilisha kwake ripoti ya uchunguzi huo katika kipindi cha siku 21 zijazo.
Pia amewaomba kuchunguza madai kuwa, maafisa wawili wakuu wa muungano wa upinzani nchini Kenya, walifaulu kudukua kompyuta za tume ya uchaguzi.
Hiyo inafuatia uamuzi wa mahakama ya juu zaidi nchini Kenya kufutilia mbali uchaguzi wa Urais wa Agosti nane kwa madai kwamba kulikuwa na makosa chungu nzima, huku mahakama hiyo ikikataa kuwalaumu moja kwa moja maafisa wakuu wa tume hiyo kwa kufanya makosa.
Tarehe ya Uchaguzi mwingine imetangazwa kuwa Oktoba 26.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Smart Ago ni jina la blog yangu ambapo blog hii nimeianzisha kwa sababu nyingi na tofautitofauti.Ambapo miongoni mwa malengo yangu ni kuwaandalia na kuwafikishia habari mbalimbali za ndani na nje ya nchi,michezo,siasa na kutoa elimu nyingine nyingi katika jamii yangu inayonizunguka ili kuweza kuwa urahisi wa wao kutohangaika kutafuta semina pengine wengine wako vijijini ata kuangalia runinga kwao ni ngumu hivyo watapata habari kwa kuandika smartago.blogspot.com popote walipo kwa kutumia simu zao za smartphone, karibuni sana na mualike na mwenzako.
No comments:
Post a Comment